Posts

Showing posts from March, 2023

WIMBO WA SHUKURANI by Joakim chawe

Image
 Wimbo: Ushukuriwe Mungu         Mtunzi: Joakim Chawe          Sauti: Joakim Chawe          Booking: 0754465961 Kwanza namshukuru Mungu, Aliyenifikisha hapa, Aliyenipa mi kibali, na kunifanya kuwa mshindi, Aliyenipa afya tele, Nakufanya niwe hodari,  Ameondoa aibu, ameweka misingi ya haki, Kwake Bwana nasimama Ndiye mwamba Ni salama Ndie mwamba Ni salama kwake Bwana nasimama. Hakuna aliyedhani, kwamba leo tungekuwa hapa, Kila siku ilikuwa kulia, machozi hayakukauka, Hatukujua kesho yetu,  Maana ya Jana tu yalitushinda, Ifikapo mapambazuko badala ya kufurahi, Tulilia Mana tuliona Ni afadhari ya Jana Mapambazuko yalipofika Tulijiuliza Ni wapi tule, ili angalau tusogeze siku Kwake Bwana nasimama Ndiye mwamba Ni salama ndiye mwamba Ni salama kwake Bwana nasimama. Ninasema Asante Bwana, Sitachoka kusema Asante Maana wewe Ni Mungu wangu Ulofanya mbingu na nchi... Habari wanafuns kwa majina naitwa Joakim, Mimi...

Mfalme masikini full episode

 MFALME MASIKINI By: Joakim artwork production Simu: 0754465961whatsapp Telegram: @joakimworkproduction255 Twitter: @joakim_chawe YouTube: Joakim work Production Katika himaya ya emperor katika miaka ya nyuma kidogo alikuwepo MFALME mmoja aliejulikana kwa jina la King Beaz. Alikuwa ni mfalme wa kwanza kushangaza ulimwengu, mbali na kwamba ufalme ulirithishwa lakini zilikuwepo sifa kadha wa kadha za yeye kuwekwa kwenye kiti kitukufu cha Cha ufalme Kama vile; hadhi, umri, Mali nyingi, majeshi ya kutosha na kadhalika. Kwa mfalme huyu ilikuwa Ni tofauti kabisa ambaye yeye alikuwa katika hali ya chini ya kiuchumi, umri mdogo na jeshi lake lilitumia silaha duni Kama vile fimbo na marungu. Licha ya hivyo himaya ya mfalme huyu ilikuwa na amani, mshikamano, na Uhuru wa kutosha, Jambo lililokuwa linawashangaza wafalme wengine duniani. Joakim work Production Ni waandishi wa vitabu na makala mbalimbali za kitaaluma kuanzia shule ya msingi mpaka kidato cha sita. Pia msimu huu wa mwisho wa semis...