WIMBO WA SHUKURANI by Joakim chawe
Wimbo: Ushukuriwe Mungu
Mtunzi: Joakim Chawe
Sauti: Joakim Chawe
Booking: 0754465961
Kwanza namshukuru Mungu,
Aliyenifikisha hapa,
Aliyenipa mi kibali, na kunifanya kuwa mshindi,
Aliyenipa afya tele,
Nakufanya niwe hodari,
Ameondoa aibu, ameweka misingi ya haki,
Kwake Bwana nasimama
Ndiye mwamba Ni salama
Ndie mwamba Ni salama kwake Bwana nasimama.
Hakuna aliyedhani, kwamba leo tungekuwa hapa,
Kila siku ilikuwa kulia, machozi hayakukauka,
Hatukujua kesho yetu,
Maana ya Jana tu yalitushinda,
Ifikapo mapambazuko badala ya kufurahi,
Tulilia Mana tuliona Ni afadhari ya Jana
Mapambazuko yalipofika
Tulijiuliza Ni wapi tule,
ili angalau tusogeze siku
Kwake Bwana nasimama
Ndiye mwamba Ni salama
ndiye mwamba Ni salama kwake Bwana nasimama.
Ninasema Asante Bwana,
Sitachoka kusema Asante
Maana wewe Ni Mungu wangu
Ulofanya mbingu na nchi...
Habari wanafuns kwa majina naitwa Joakim,
Mimi niwandishi wa vitabu na makala mbalimbali za kitaaluma kuanzia ngazi ya shule ya msingi mpaka kidato Cha sita.
Pia Ni mtunzi na mwandishi wa nyimbo, mashairi aina zote, simulizi, visa na Mikasa.
Unaweza kujifunza zaidi kupitia YouTube channel kwa jina la Joakim work Production
na WhatsApp namba: 0754465961
tellegram:@joakimworkproduction255
Asante see you at the top.
Comments
Post a Comment